Ann Kansime: Nilichangia bwanangu ili anioe - RAHA ZA KITANDANI

Ann Kansime: Nilichangia bwanangu ili anioe

- Kansiime alisema alichangia bwanake mahari yake ambapo ni kinyume cha desturi ya Afrika
- Ndoa ya wawili hao ilidumu kwa miaka mitano kabla ya misukosuko na akapatiwa talaka
- Mchekeshaji huyo alisema wakati huo alikuwa bado hajijui
Mchekeshaji mashuhuri kutoka nchini Uganda Ann Kansiime amefichua maswala ya ndoa yake ambayo huenda yalisababisha kuvunjika kwa uhusiano wao.
Kansiime alisema kuwa yeye alichangia mumewe ili aweze kumlipia mahari.
Ann Kansime: Nilichangia bwanangu ili anioe
Mchekeshaji Ann Kansiime. Picha: Ann Kansiime
Source: Facebook
Kulingana na mila na desturi za Kiafrika, ni mwanamume ambaye anafaa kujipanga na kuweza kumlipia mwanadada ambaye anataka kumuoa mahari.
Akiongea kwenye mahojiano na Nana Gaga, Kansiime alisema penzi lilimsukuma kiwango cha kuamua kuongezea mumewe mali ili afike kiwango cha mahari.Kansiime alikuwa ameolewa na Gerard Ojok kwenye ndoa iliyodumu miaka mitano kabla ya kuvunjika mwaka wa 2017.
"Nilisema mtu alinioa na akaamini, na yeye pia kusema alinioa. Baadaye, nikagundua kuwa kuolewa ni mwanaume kuamka kwa miguu yake, anakulipia mahari, anakupeleka kanisani na kisha anakuoa ... hakuna kama hilo lilifanyika kwangu," Kansiime alisema.
Alisema penzi linapomuingia msichana, basi linaweza kumzungusha pakubwa.
"Unajua ukimpenda mtu, utafanya chochote ili aweze kukupata ... aweze kukulipia mahari. Aweze kupata mahari hiyo," alisema.
Mchekeshaji huyo alijipatia jina kupitia vipindi vyake kama vile 'Don't Mess with Kansiime' ambavyo vimekuwa maarufu.