ZIFAHAMU NJIA KUU NNE ZA KUPATA MTOTO WA KIKE. - RAHA ZA KITANDANI

ZIFAHAMU NJIA KUU NNE ZA KUPATA MTOTO WA KIKE.





dunia inakwenda kasi sana siku hizi, kiasi kwamba imefika hatua mtu akizaliwa mwanaume sio lazima kwamba atakufa mwanaume. teknolojia imefika mbali sana kiasi kwamba watu wana maamuzi juu ya maisha yao, miili yao, watoto wao na machague mengi tofauti tofauti. moja ya maswali ambayo nimekua nikiulizwa sana ni jinsi ya kuchagua jinsia ya mtoto. nimeshawahi kuongelea jinsi ya kupata mtoto wa kiume leo ntaongelea wa kike. hivyo leo naenda kuongelea njia za kitaalamu zinazoweza kukufanya kuongeza uwezekano mkubwa wa kupata mtoto wa kike.

fanya mapenzi siku moja, mbili au tatu kabla ya siku ya yai kushuka: yai la mwanamke hua linashuka mara moja tu kwa mwezi kulingana na mzunguko wa mtu husika, mfano mzunguko wa siku 28 siku ya 14, mzunguko wa siku 30 siku ya 16, mzunguko wa siku 32 siku ya 18 na kadhalika. kufanya mapenzi siku hizi kutafanya mbegu za mtoto wa kiume ambazo siku zote hufika mapema kwenye kizazi, zikute yai la mama na kurutubisha hivyo kutoa mtoto wa kiume hivyo jinsi ya kupata mtoto wa kike hapa ni kufanya mapenzi siku mbili au tatu kabla ya hii siku hii ile mbegu za mtoto wa kiume ambazo huishi muda mfupi zife zibaki zile za mtoto wa kike.kama mzunguko wako haueleweki ni bora kuangalia kama kuna tatizo ili uweze kuusoma vizuri.unaweza kutumia virutubisho vya kufanya kazi hii kwanza.

mwanamke ajizuie usifike keleleni; uke wa mwanamke una tindikali nyingi sana ambazo huua kirahisi mbegu za jinsia ya kiume na kuacha zile za jinsia ya kike hivyo mwanamke akifika kileleni tindikali hiyo hupotea sababu ya maji mengi kumwagika na hii huweza kushindwa kuua mbegu za mtoto wa kiume.

fanya mapenzi mara kwa mara; mwanaume anayefanya mapenzi mara kwa mara anapunguza ukomavu wa mbegu zake hivyo anakua kwenye nafasi nzuri ya kutengeneza mbegu ambazo zinatoa mtoto wa kike kuliko mtoto wa kiume ambaye anahitaji kupatikana kwa mbegu zilizokomaa sana.

tumia staili za ngono zenye muingilio mdogo; staili za zanye muingilio mdogo kama mwanamke kutangulia chini na mwanaume kuja juu hua na muingilio mdogo hivyo mbegu za mwanaume humwagwa juu juu sana na kusababisha zile za kiume kushindwa kusafiri na vizuri na kufa hivyo za mtoto wa kike kuwahi na kuleta mtoto wa kike.
kwa maelezo zaidi fungua hapa usome