WAJUE MAADUI WA MWANAMKE KUFIKA KILELENI(1) - RAHA ZA KITANDANI

WAJUE MAADUI WA MWANAMKE KUFIKA KILELENI(1)


Si utundu na ujanja wa mwanaume tu unaomwezesha mwanamke kupata utamu wa kufika kileleni (mshindo, orgasm, coming) bali mwanamke pia anahusika.
KUFIKA KILELENI NI NINI?
Ni kiwango cha juu kabisa cha utamu, hisia, raha, msisimko wakati wa tendo la ndoa wakati ambapo misuli ya uke au uume hukaza.
Kwa mwanaume huambatana na kutoa manii (ejaculation). Wengine wakifika kileleni hupiga kelele sana, wengine huongea maneno ovyo ovyo hata matusi, wengine huzimia kabisa.
Wengine huwakwida wapenzi wao kama vile kibaka, wengine hutulia kimya na kupitilia za usingizi na wengine ukiwauliza wanasema mahali walikuwa ni kama vile walikuwa hewani, ilimradi tu ni raha na utamu.
Ukweli Mwenyezi Mungu alitupa zawadi ya ajabu na hii ni kujulisha kwamba Mungu alituumba tena kwa namna ya ajabu, pia wengine huita kufikia mshindo, wengine huita coming n.k Pia wapo ambao kwa tendo moja la ndoa huweza kufika kileleni zaidi ya mara moja.
JE, MWANAUME NA MWANAMKE WOTE HUFIKA KILELENI SAWA?
Kwa wanaume kufika kileleni ni suala ambalo ni automatic, halina mjadala, kitu cha msingi kwake ni kujitahidi asifike mapema kileleni ili amfikishe mke wake pale anatakiwa kufikishwa.
Kwani mara nyingi mwanaume akifika kileleni hupoteza uwezo wa kuendelea na tendo. Katika nchi zilizoendelea kama USA na Canada utafiti mwingi unaonesha kwamba Asilimia 15 % ya wanawake hufika kileleni mara zote.
Asilimia 48 % ya wanawake mara nyingi hufika kileleni. Asilimia 19 % ya wanawake ni kawaida kufika kileleni lakini si mara nyingi Asilimia 11 % ya wanawake ni nadra sana kufika kileleni na Asilimia 7% ya wanawake hawajawahi kufika kileleni na hawajui ni kitu gani.
Hapa ni wanawake kutoka nchi zilizoendelea ambako elimu kuhusu mapenzi ni kubwa sana.
Je, kwetu nchi zilizogoma kuendelea hali itakuwaje? Ukizingatia wanaume wengi bado hawajajua nini wanawake wanahitaji ili kufikishwa kileleni?
Pia kuna baadhi ya wanawake ambao hata wasipofika kileleni hawana shida wanaridhika tu bora maisha yanaenda.
NINI KITU MUHIMU KUHUSU MWANAMKE KUFIKA KILELENI?
Wanawake wanaweza kuendelea kupata utamu hata baada ya kufika kileleni hivyo ni jukumu la mwanaume kuhakikisha anabaki ndani ya uke hadi anahitimisha tendo zima (conclusion) angalau kwa dakika 10 au 15 ndo ukimbie kuoga au kupiga usingizi.
Siyo kumwacha kiumbe wa watu kwenye mataa akiugulia kumuondolea utamu na raha. Tendo la ndoa huwa ni la kuridhisha sana hasa pale mume anapomfahamu vizuri mwanamke na kile anahitaji kwa kumfanyia utundu wote wa kuchokonoa sehemu zote ambazo zinaweza kumhakikishia kwamba atafika kileleni.
Lakini pia mwanamke anasehemu kubwa sana ya yeye kujihakikishia anafika kileleni si mwanaume tu ni suala la wote.
Kutoka na makala hii kuwa kubwa, nakusihi mpenzi msomaji wa blogu ya ASILI ZETU endelee kutembelea kwa muendelezo wa makala hii muhimu sana kwenye suala la mahusiano.