MWALIMU NAE ANATAKA (1) - RAHA ZA KITANDANI

MWALIMU NAE ANATAKA (1)



Mwaka 1998, ilikuwa ni Jumapili mida ya saa kumi jioni, Eric kijana mwenye umri wa miaka kumi na tisa, alionekana amevalia kimichezo, yani bukta ndevu nyekundu na tishert ya kijivu, chini alivalia rubber za michezo kama zile za wachezaji wa mpira wa kikapu wa marekani wanazovaaga, licha ya kuvaa begi lake dogo la mgongoni, pia mkononi alikuwa amebeba mpira wake wa kikapu, Eric alikuwa anakimbia akikatiza mitaa ya Mahenge B kuelekea mjini kwenye uwanja wa Zimani Moto ambako kwa sasa ndiko anakofanyia mazoezi, na kwa sasa alishaanza kujipatia marafiki kwenye mchezo huo ambao alikuwa hodari sana, hata kwenye shule zote sita za bweni alizowahi kusoma kabla ya hii shule ya kutwa aliyopo sasa, toka kidato cha kwanza mpaka kidato hiki cha tatu alichopo kwa sasa, alikuwa akitegemewa sana kwenye timu za basketball za shule na mtaani, pindi akiwa likizo, Eric aliendelea kukimbia akipishana na watu ambao walikuwa au wanaenda au kutoka matembezi, katika mtaa huu uliochangamshwa na sehemu za kufanyia biashara, zikiwemo maduka na mabucha ya nyama, pia mabar na sehemu za burudani, music mkubwa pia ulisikia ukichangamsha mtaa.

Wakati Eric anaendelea kukimbia, na sasa alikuwa anakatiza nyumba za mwisho za mtaa huu wa Mahenge B ili kuinga kwenye usawa wa uzio mkubwa sana wa ofisi za idara ya maji ya mkoa wa Ruvuma, ndipo aliposikia sauti ya mwanamke ikiita jina lake, “Wewe Eric!!!!!!” hapo Eric akageuza shingo na kutazama nyuma kumtazama mwanamke aliyekuwa anamuita, na alipomuona alijikuta anasimama kabisa, “Hoooo Mwalimu Sarah, shikamoo mwalimu” alisalimia Eric akitazama mwalimu ambae sasa alikuwa amemsogelea kabisa, “Poa Eric, naona unaenda mazoezini” aliongea huyu ambae Eric anamuita mwalimu akiwa ameachia tabasamu la kuvutia lililosababisha muonekano wa mwalimu huyu kuwa wakuvutia zaidi huku akimtazama usoni mwanafunzi wake Eric kwa macho yake ya ajabu ambayo akikutazama unaweza kuhisi anakubembeleza, “Ndio mwalimu, naenda Zimani Moto hapo” alijibu Eric huku akikwepesha macho yake yasikutane na macho ya mwalimu Salah.

Huyu anaitwa Sarah Mwakapeje, ni msichana mrembo sana mwenye umri wa miaka ishirini na tano, ni mwalimu katika shule ya sekondari ya Luhuwiko ambayo ipo nje kidogo ya mji karibu na kambi moja la jeshi, uzuri na urembo wa mwalimu huyu uliwachanganya wengi sana hapa mjini Songea, ukiachilia wanaume wenye umri kama wake ambao wengi wao walikuwa ni walimu wenzake pia vijana kwa wazee watu wazima wa mtaani nao walimmendea sana mwalimu Sarah ambae ana miezi miwili tu! toka alipoanza kufundisha shule hii ya Luhuwiko, lakini mwalimu Sarah alikataa offer za wanaume hao, siyo kwamba hakuwai kuwa na mpenzi, mwalimu Sarah ambae ameajiliwa kwa muda hapo suleni, ndio kwanza alikuwa amemaliza chuo cha ualimu alikokuwa anasomea diploma, na sasa alikuwa anasubiri ajila za selikari, alikuwa ametengana na mpenzi wake Jacob aliyekuwa nae kwa muda wa miaka mitatu katika chuo cha ualimu Nambambo huko Nachingwea mkoani Lindi, na wametengana baada ya kumaliza chuo na kila mmoja kuelekea upande wake, wakati Sarah akielekea Songea kwa wazazi wake, Jacob aliekea Kilimanjaro kwa wazazi wake pia.

“Samahani Eric maana nimekuchelewesha, ila nina shida kidogo” aliongea mwalimu Sarah akimkazia macho Eric huku akitabasamu, “Usijali mwalimu, shida gani hiyo?” aliuliza Eric akijichekesha huku akikwepesha macho yake yasikutane na macho ya mwalimu wake huku moyoni akishangaa sana kitendo cha mwalimu huyu wa kidato cha pili anayesifika kwa urembo pale shuleni, isitoshe hakuwa na mazoea na mwalimu huyu, tena alikuwa na uhakika mkubwa kuwa mwalimu huyu hakuwa anamjua lakini leo alishangaa kuwa anamfahamu hadi jina.

“Naomba uniazime fedha kidogo, nitakurudishia Jumatano” aliongea mwalimu Sarah kwa sauti yake nyembamba na ya kuvutia, “Sawa mwalimu, sijui ni kiasi gani?” aliuliza Eric huku moyoni akiwa bado anashangaa leo kufanya maongezi kama haya na mwalimu huyu ambae kila mwanafunzi pale shuleni kwao alikuwa anatamani kupata nafasi kama ile, “Nahitaji elfu ishirini, yani nimeishiwa vibaya na mwisho wa mwezi bado mbali sana” alisema mwalimu Sarah huku akisogea karibu kabisa aliposimama Eric na kusababisha kila mmoja aipate harufu ya mwenzie, “Hakuna tatizo mwalimu, hapa nina fedha kidogo tu!” aliongea Eric huku akitoa begi lake mgongoni na kufungua mfuko wa pembeni, akaibuka na fungu la noti za elfu moja moja, akazihesabu tano, “Chukuwa hizi kwanza halafu kesho shuleni nitakubebea kumi na tano” aliongea Eric huku akimpatia mwalimu zile fedha na kubakiwa na noti tano mkononi mwake, “Ahsante sana Eric, yani hapa leo umenisaidia sana” alisema Sarah huku akinyoosha mkono wake kupokea zile fedha toka kwa Eric, na wakati anazipokea akakamata mkono wa Eric na kuuminya kidogo kitendo kiichomstua kidogo Eric na kumtazama mwalimu Sarah usoni, akakutana na tabasamu mwanana lililotawala usoni kwa mwalimu huyu mrembo huku akimalizia kwa kumkonyeza kwa jicho lake la kulia, kitendo hicho kilimsisimua sana Eric na kujikuta akiduwaa kama ameona treni likitembea baharini.

“Eric usisahau kesho uniletee” Eric aligutuka toka kwenye bumbuwazi na kumuona mwalimu wake akimuachia mkono na kugeuka kisha kurudi alikotokea, yani Mahenge, “Sawa mwalimu nitakuletea” alijibu Eric akiwa ameganda anamtazama mwalimu Sarah ambae alikuwa anamuona kwa nyuma, Eric aliweza kuyaona makalio ya mwalimu huyu yakiwa ndani ya gauni pana lililoshindwa kuficha pembe la ng’ombe na kuruhusu makalio hayo yaonekane yanavyotikisika, “Mh! huyu mwalimu anahatari huyu” aliwaza Eric akiwa bado ameganda anamtazama mwalimu wake jinsi alivyojaliwa msambwanda wa maana, Eric alimtazama mwalimu wake amba alitembea kama hatua kumi hivi kisha akageuka na kumtazama Eric ambae bado alikuwa anamshangaa, kama vile mwalimu Sarah alijua anachokishangaa mwanafunzi, yeye akatabasamu na kumpungia mkono, Eric nae akapunga mkono na kugeuka haraka kisha akaanza kukimbia kuelekea Zimani Moto.

Huyu anaitwa Eric Charles, ni mtoto wa kwanza kati ya wawili wa mzee Charles na mke wake, Eric na dada yake Agnes ambae ndio kwanza alikuwa darasa la saba, wamebahatika kuzaliwa katika familia yenye uwezo mkubwa wa fedha, maana wakati baba yao akiwa mkurugenzi wa TASM(Tanzania Secret Mission), mama yao alikuwa anajihusisha na biashara mbalimbali ikiwemo biashara ya maduka matatu ya nguo na bidhaa za majumbani, pia alikuwa anamiliki salon kubwa sana ya kike katikati ya mji wa Songea ambayo humwingizia fedha nyingi sana kutokana na wanawake wengi kupendelea pale kwa ajili ya kujipamba na kutengeneza nywele zao, kiukweli wazazi hawa walikuwa wanawapenda sana watoto wao, waliwafanyia vitu vingi sana vizuri ili wawe na furaha, lakini licha ya kufanyiwa mambo mengi mazuri na wazazi wake, Eric alikuwa tofauti sana na wenzake ambao ni watoto wa matajiri, hakuwa na majisifu wala hakukujiona wa pekee, alikuwa mcheshi na msikivu, aliongea na kila mtu, lakini tatizo lake yeye alikuwa mkorofi sana hasa anapokorofishwa, ndio sababu ya kufukuzwa katika shule sita za bweni alizowahi kusoma kiasi cha wazazi wake kuamua kumhamishia shule ya kutwa ambako nako kwa mwezi mmoja huu aliokuwepo hapa shuleni, ameanzisha tabia ya kukacha baadhi ya vipindi akienda kujificha Pacha Nne kwenye mgahawa wa rafiki yake David uliopo Pacha Nne pembeni kidogo ya shule hiyo ya Luhuwiko ikitenganishwa na barabara kuu ya mtaa wa Lizabon.

Eva na Amina walikuwa wametulia kwenye jukwaa moja usawa wa kiwanja cha netball, ni moja ya kiwanja kati ya viwanja vinne vya michezo kinachokusanya mashabiki wengi sana hasa wakiume, humu ndani ya uwanja wa Zimani Moto uliokusanya viwanja vya football, volyball na basketball, yani ukiachilia uwanja wa netball ambao umejikusanyia washabiki wengi kutokana na mchezo huo wa netball kuchezwa na wanawake waliovalia nguo fupi, “Kumbe kunakuwa na watu wengi sana!” aliongea Eva kwa sauti ya mshangao akionesha kupendezwa na mazingira yale, “Yani unakosaga uondo kweli kweli” alijibu mwenzie ambae ndie Amina rafiki yake mkubwa, kiukweli licha watu kufuatilia mchezo wa netball, lakini asilimia ya wanaume wengi walikuwa wakimtazama Eva wakiacha kutazama mpila netball.

Wakati Eva na Amina wanaendelea kuongea mala wakashangaa wakimuona kijana mmoja aliyevalia kinadhifu akija na kukaa karibu yao, “Mambo vipi warembo?” alisalimia yule kijana, huku akimtazama Eva kwa macho ya matamanio, “Safi” alijibu Amina na kumfanya yule kijana amtazame Amina kwa macho makali kisha akamtazama tena Eva, “Niambie Eva mambo yanaendaje?” aliongea tena yule kijana, lakini hapo ni kama aliwaambia wakina Eva waondoke, maana Eva alisimama na kumshika mkono Amina kisha wakaanza kuondoka kuelekea kwenye jukwaa la upande wa mpira wa kikapu.

Huyu anaitwa Eva Jackson, mwanafunzi wa kidato cha tatu shule ya sekondari ya kutwa ya Luhuwiko, wengi wanapenda kumuita Eva Muzungu kutokana na rangi yake ya kichotara ambayo ilizidisha uzuri wake maradufu, ukiachilia umbo lake la mwili lililokaa vyema na kumfanya kila mwanaume atamani kumuona akiwa mtupu, ni mwanamke ambae anajiheshimu na kuogopa wanaume siku zote toka alipovunja ungo miaka miwili iliyopita na kusababisha mpaka anatimiza miaka kumi na tisa kitumbua chake kiwe hakijaguswa na mwanaume yoyote, siyo kama kuna mtu alikuwa anamsimamia juu ya hilo, lakini yeye mwenyewe hakuona mwanaume wakumpatia kitumbua chake, Eva ambae ailikuwa anaishi na mama yake kwenye nyumba yao mtaa wa Mfaranyaki, ukweli ni kwamba hakuwai kumuona baba yake toka akiwa darasa la pili, ambapo baba yake raia wa uingereza aliomaliza mkataba wake wa kuwepo nchini Tanzania ambapo alikuwa mkoani Ruvuma kama msimamizi wa mitambo ya kukaushia na kusindika tumbaku kwenye kampuni binafsi ambayo hata mama yake Eva alikuwa akifanya kazi hapo, na ndipo walipokutana na kuwa wapenzi mpaka kupata ujauzito wa Eva.

Lakini bwana Jackson hakuondoka hivi hivi, aliwaachia nyumba kubwa na nzuri pia fedha ambazo ziliwasaidia kwa malezi ya Eva, hata miaka saba baadae mama Eva alipopunguzwa kazini kutokana na tikisiko la uchumi, alijikuta akiendelea vizuri kimaisha japo siyo kwa kiasi kikubwa kwa kufungua duka nje ya nyumba yake ambayo hipo pembeni ya babarabara ya mtaani kwao, duka lililo wawezesha kupata mahitaji muhimu ya kila siku huku wakikosa mambo ya ziada kama familia nyingine zenye uwezo, maana lifikia kipindi Eva alikosa hata fedha ya nauli au ya kula shuleni, lakini licha ya hayo, Eva hakuingiwa na tamaa kwa vishawishi ambavyo alikuwa anakutana navyo kila siku kutoka kwa wanaume wa kila lika, wazee watu wazima na vijana hata wanafunzi na walimu wenzake, huku baadhi ya walimu wakitumia hata ubavu na vitisho kumladhimisha awapatie kitumbua.

Usikose sehemu ya Pili(2)