Amerudi safari lakini hajanigusa wakati nahitaji dozi - RAHA ZA KITANDANI

Amerudi safari lakini hajanigusa wakati nahitaji dozi



Mimi ni mwanamke ambaye nina mume na watoto kadhaa, ninaishi na mume wangu ila yeye muda mwingi huwa yuko mkoani kikazi zaidi.
Kuna wakati namaliza muda mrefu sana bila kuonana naye, kama mwanadamu Napata hamu haswa yakukutana naye faragha ila kwa sababu ya majukumu na umbali basi nakuwa mpole na kumvumilia.

Hivi karibuni mume wangu aliniambia kuwa siku fulani anarudi nyumbani, mwanamke niliyefunzwa nikafunzika, nilijiandaa kuanzia kihisia, kimazingira, mavazi, chakula na mambo mengi ili kumuhamasisha zaidi mume wangu atakapofika tuingine moja kwa moja kwenye dimbwi la mahaba.
Nilijaribu kufanya kila aina ya njia ili mradi kumvutia na kumshawishi anipe dozi kwani mwenzane nilikuwa nahitaji sana kwa muda mrefu lakini…
Image result for black he doesnt want sex
Kilichonishangaza alipofika alikuwa bize na mambo yake, hana hamu na mimi kama nilivyofikiria, wala shipa lake hata halimchezi, hata kushtuka kuwa mkewe hajanipa dozi siku nyingi!
Niliumia sana, nikavumilia nikiamini labda usiku atanipa haki yangu lakini usiku nao wala hajaniuliza wala kutaka chochcote, inauma sana kwa mpenzi hasa mumeo.
Baada ya kukuchana mchana wake ndiyo eti anaonesha kama anataka mambo yetu labda kwa sababu alijua nimechukia na kununa!
Hali hii inaniumiza sana, naiona ndoa yangu kama imeanza kuwa chungu,