SIMU ZA MKONONI NI MATATIZO KATIKA MAHUSIANO? - RAHA ZA KITANDANI

SIMU ZA MKONONI NI MATATIZO KATIKA MAHUSIANO?


Habari wapendwa karibu mara nyingine tena katika blog yako hii uipendayo tuzungumze mambo yanayotuzunguka katika maisha halisi tunayoishi (Duniani) endelea….
Leo napenda tujadiliane suala la simu za mkononi. Suala hili bilashaka limeshazungumzwa mara nyingi sana katika vyombo mbali mbali vya habari, simu za mkononizina faida nyigi tu ila wahenga walisema “kila lenye faida halikosi hasara”, lakini mimi napenda kuingia ndani zaidi na kulihusisha na suala la mahusiana kati ya wapendanao.

Unawezaje kuyafanya  mahusiano yako yadumu na yasivunjike kwa sababu tuu ya simu yako au ya mwenza wako?
Watu wengi sana wamekuwa wakijikuta katika wakati mgumu kwa sababu ya kitu hiki kidogo, simu!!! Hebu jiulize! “kwanini wewe unamiliki simu yako na ya mpenzi wako? kwanini humuamini? kwanini nawe pia hujiamini?  Je kama anakupenda kwa dhati anaweza kukudanganya? kwa nini usimpe nafasi ajitambue kuliko kuwa mlinzi wa simu yake? Unahisi wewe ukijua anawasiliana na nani kutwa nzima ndo utakuwa na furaha maishani au utaongeza matatizo moyoni mwako na katika mahusiano yenu?
Maswali hayo machache tujiulize kabla hatujaenda mbali. WHY? KWANINI?
Katika hali ya kawaida tu ukikagua simu ya mweza wako kila wakati utajikuta badala ya kupata faraja moyoni unajikuta unapata stress ambazo hazina mpango!! Unaumiza moyo wako maana utajikuta unagundua vitu vingi vya ajabu na mahusiano yanaanza kuvurugika!



                                                        
                                                             JE! NI NINI SULUHISHO?

Uaminifu ni kitu kizuri, muonyeshe kuwa unamuamini sana. usimfuatilie kupita kiasi hasa katika simu yake ya mkononi. Mwache awe na uhuru na simu yake, muonyeshe kuwa bila yeye unaweza kuishi maana ukifuatilia sana simu yake, utaumia na atabaini kuwa bila yeye hujiwezi sikio wala ndewe!!


MAMBO AMBAYO WANAUME WANAKOSEA WAKATI WA KUTONGOZA