UNAMNYIMA MUMEO TENDO LA NDOA, HALAFU UNAJISIFU UKO KWENYE NDOA,,,, - RAHA ZA KITANDANI

UNAMNYIMA MUMEO TENDO LA NDOA, HALAFU UNAJISIFU UKO KWENYE NDOA,,,,


TENDO LA NDOA linachukua asilimia nyingi sana katika kukamilisha Neno Ndoa, na ndoa wala haiishii kwenye kuvaa pete mbili, na shela peke yake,,, ndoa inakamilishwa na TENDO LA NDOA ambalo  wanawake wengi siku hizi wamekuwa WAKIWADORISHIA WAUME ZAO, na kuwapa kwa mahesabu,, had watakapofurahi wao ndio wanalitoa kwa moyo, au akiona ana shida ya kitu flan bas ndio analitoa kwa mumewe,,, lakini mume anapomuhitaji, yeye hayuko teyar, eti anaendeshwa na mood,  kwani ni MRADI HUO???

  mimi nawashangaa sana wanawake mnaowapa waume zenu mapenzi kwa kuwapimia, wakat kwa  christian tumeambiwa MKE HANA MAMLAKA JUU YA MWILI WAKE  ISIPOKUWA MUMEWE, NA MUME  HANA MAMLAKA JUU YA MWILI WAKE ISPOKUWA MKEWE. Sasa wewe ndugu yangu, unamuhesabia mumeo  kwa mpango upi?,,, unavyomkatalia unafikiri wapi ataenda kulimaliza  haja ya mwili wake, wakat wewe ndio wake na upo hapo kwa ajili yake?/


Unaacha mumeo anatamani tamani hovyo uko nje, kila mwanamke atakaekatiza mbele yake mumeo  anamtamani, ufanisi wa kazi zake umepungua kichwa kimejawa na mawazo, wewe upo, tu unakalia kusafisha pete zako za ndoa kila siku ujulikane mke wa flan,,,,, unadhani hiyo ndio ndoa?? mimi huwa napenda kusema ukiletewa taarifa MUMEO ANACHEPUKA, BASI CHA KWANZA INABID UJIULIZE, MIMI KAMA MLINZI WA MUME WANGU, NILIKAA KWENYE NAFASI YANGU KUHAKIKISHA NAMLINDA INAVYOSTAHILI??? AU NILISHINDWA KUMPA CHAKULA CHA KUTOSHA IMEBID AKAJITAFUTIE MWENYEWE HUKO NJE??


 Hivi ni wapi atakula chakula kilicho salama, ni NJE Atakapokwenda kutafuta mwenyewe, au ni nyumbani anapopikiwa na Mlinzi wake?  biblia haikukosea ilipogawa nafasi hizi ,,, mwanaume na nafas zake, mwanamke na nafasi zake,,,, inashangaza sana kuona wanawake wanasahau nafas zao ambazo ndio NYINGI SANA za kuleta uponyaji katiak ndoa zetu,,,, wewe unakaa wiki tatu, hutaki kuguswa, wengine mnaweka mashuka mawili kabisa kitandani kila mtu na lake,, wakat MMESHAKUWA MWILI MMOJA, AU UMESAHAU HAYO?

HALAFU NYIE NYIE NDIO WA KWANZA KUSEMA WAUME ZENU WANACHEPUKA,, WATAACHAJE SASA WAKATI PALE WANAPOSTAHILI KUPATA CHAKULA HAKUNA,, WAFE NJAA?



MUNGU atusaidie sana wanawake kuweza kutambua wapi tutanakiwa kusimama kama kina mama katika kujenga ndoa zetu,,, tendo la ndoa lina faida nyingi sana kama tulikifanywa kwa kupenda na kila mtu kujitoa kwa ajili ya mwenzie,

IJUMAA IJAYO TUTALITAZAMA TENDO HILI NA FAIDA ZAKE KWA UJUMLA,

MUNGU ATUSAIDIE SANA KUWEZA KUTAMBUA YATUPASAYO KUTENDA.. MIMI NAAMINI  KABISA KAMA MAMA UTASIMAMA IMARA, KWENYE NDOA YAKO, UKATAMBUA NAFAS YAKO KAMA MAMA, WA FAMILIA, NZIMA, WEWE NDIO CHANZO CHA BARAKA NDANI KWAKO,
NA NAFAS HIZO ZINATEGEMEANA, UKIACHA MOJA BAS MBELENI LAZIMA KUNA INGINE NAYO ITAKUSHINDA TU,,,,,

MALALAMIKO JUU YANDOA YAMEKUWA MENGI SANA WALIOPO GROUP YA (COMFORT ZONE WANAFAHAMU) Kila siku wanawake wanalia sana, na ndoa zao, lakini nyingi zao ukichunguza utakuja kugundua kwamba SISI WENYEWE NDIO CHANZO CHA SHIDA NA SISI SISI NDIO WA KWANZA KULALAMA
SIO SAWA,,,

MUWE NA WEEKEND NJEMA